Ijumaa, 20 Juni 2014

hskjkjxsx

“IMANI IOKOAYO IMANI IKOMBOAYO NI NINI?”



 “IMANI IOKOAYO IMANI IKOMBOAYO NI NINI?”

Yakobo 2:14 “Ndugu zangu,yafaa nini,mtu akisema kwamba anayo imani,lakini hana matendo?je!ile imani yaweza kumwokoa?”  ile imani; neno hili ile imani lina maana ni aina gani ya imani inayookoa.Sio kukubaliana kwa akili na kweli ya biblia kuhusu Mungu Yakobo 2:19 “Wewe waamini ya kuwa Mungu ni mmoja;watenda vyema.Mashetani nao waamini na kutetemeka” Imani iokoayo hutenda na kutii.Uwe na upendo wa amri za Mungu na utii Yakobo 2:20 “Lakini wataka kujua,wewe mwanadamu usiye kitu,kwamba imani pasipo matendo haizai?” Rum 10:9—10 (9.Kwa sababu ukimkiri Yesu kwa kinywa chako kwa kuwa ni Bwana,na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu,utaokoka 10.Kwa maana kwa moyo mtu uamini hata kupata haki,na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu)

Imani humtii Mungu kwa moyo usio kichwa  ?” Rum 10: “Kwa maana kwa moyo mtu uamini hata kupata haki,na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu” Efeso 2:8—9,Rum 16:26 (Ikadhihirishwa wakti huu kwa mandiko ya manabii,itajulikana na mataifa yote kama alivyoamuru  Mungu wa milele ili waitii imani) Efeso 2:10 “Maana tu kazi yake,tuliumbwa katika Kristo Yesu,tutende matendo mema,ambayo tokea awali Mun gu aliyatengeneza ili tuenende nayo” Imani iokoayo ni kipawa cha Mungu.(Isaya 61:10)ni kuvikwa na kufunikwa (Isaya 64:6,Luka 43:48.Ebra 7:22,Ebra 6:6,Ebra 12:24,Ebra 4:10)sasa yapo maagano na mikataba
Agono na mkataba sio kitu kimoja kama watu wanavyodhani,Mkataba ni kazi ya binadamu na Agano ni kazi ya Jehova 1 Yoh 1:8—9 “Tukisema kwamba hatuna dhambi,tunajidanganya wenyewe,wala kweli haimo mwetu 9.Tukiziungama dhambi zetu,yey ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambie zetu,yeye hutasafisha na udhalimu wote”lazima tuanze kwa toba iwapo tunataka ukombozi wa kweli Lawi 17:11 “kwa kuwa uhai wa Mwili u katika hiyo damu;nami nimewapa ninyi hiyo damu juu ya madhabahu,ili kufany upatanisho kwa ajili ya nafsi zenu;kwani ni hiyo damu ifanyayo upatanisho kwa sababu ya nafsi” kiri damu ya Yesu  1 Yn 1:7 “Bali tukienenda nuruni,kama alivyo katika nuru,twashirikiana sisi kwa sisi na damu yake Yesu,mwana wake,yatusafisha dhambi yote” Ulinzi Kumb 28:7 “Bwana atawafanya adui zako wainukao juu yako kupigwa mbele yak;watakutokea kwa njia moja,lakini watakimbia mbele yako kwa njia saba”( 1kor 2:10) Roho (Rum 8:26 “) Kusamehe (Mt 6:14) Kisasi (Yer 15:15) Uponyaji (Zab 107:20)kukanyaga nguvu za adui.Angusha ngome( Yoshua 6:20)
Ni hakika kwamba tumetoka katika jamii tofauti zilizo chini ya maagano mbalimbali ambayo yamevuta laana mbalimbali sasa kabla ya kuendelea sana ni vyema tuone na kujua laana maana yake ni nini?LAANA ni maneno yaliyozungumzwa au kunuizwa yenye uwezo katika ulimwengu wa roho ya kuharibu hatima ya mtu au ukoo na katika laana hizi zipo aina saba za laana
1.       Kuna laana ya Mungu
2.       Kuna laana ya Manabii
3.       Kuna laana ya Torati
4.       Kuna laana ya  shetani
5.       Kuna laana ya ukoo
6.       Kuna laana ya kujifanyia
7.       Kuna laana ya kushirikishwa
Na hizo zote zina nguvu ya kuharibu japo laana ya Mungu ni ngumu sana na laana ya manabii kuliko laana ya shetani na torati (sheria) ni budi mtu atakaye kutoka katika laana au anayetaka ukombozi katika laana kwanza awe na imani ikomboayo Biblia inatuambia katika Rum 1:17 “Kwa maana haki ya Mungu inadhihirishwa ndani yake,toka Imani hata imani,kama ilivyoandikwa,mwenye haki ataishi kwa Imani” Hivyo tunatoka Imani hadi Imani,Ushindi hadi Ushindi kwa Ushindi wa Yesu.  1 Kor 15:57 “Lakini Mungu na ashukuriwe atupae kushinda kwa Bwana wetu Yesu Kristo” iyo safari ya kutoka katika laana na kuingia katika Baraka inaanzia katika ushindi wa Imani (Gal 3:14—15) hatuna hofu tena wla mashaka yeyote katika Agano alilotupatia Mungu nalo linajengwa katika uaminifu katika kutii Imani  Rum 16:26
Hapo kukwatishwa tamaa na adui kwa vikwazo anavyoweka katika njia zetu sio mambo yanayoweza kujenga maisha yenye nguvu na ushindi.Sisi tumepata msaada ulioshuka toka juu.Ushindi wa Yesu ndio tumepewa yeye aliyekubali kuwa laana,hapa lazima uwe makini laana inayoongoza kuondoka baada ya mtu kuingizwa katika familia ya Mungu ni ile ya Torati (Gal 3:13 “Kristo alitukomboa katika laana ya torati,kwa kuwa alifanywa laana kwaajili yetu;maana imeandikwa ,Amelaaniwakila mtu aangikwaye juu ya mti.)Ibilisi hana uwezo tena wakuwashinda wala kuwadanganya watu wa Mungu.(yohana 1:12 Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu,ndio wale waliaminio jina lake;) Hapo ndipo wote waliompokea wana kuwa baba na kupewa uwezo,mamlaka,ruksa,haki(exsosia).Ibilisi anawadanganya  wale tu wasio jua wao niwakina nani katika kristo Yesu.Ushindi wa Yesu ufufuo wa Yesu tumepewa tumehesabiwa haki ya kuaushindi  wetu kwa imani katika neema yake (yohana 8:32 tena mtaifahamu kweli,nayo hiyo kweli itawaweka huru. Katka ms 36 basi mwana akiwaweka huru mtakuwa huru kweli kweli.
Tumewekwa huru mbali na misri na uovu wake,na mizigo yake (Ebr 2:14-15 Basi,kwa kuwa watoto wameshiriki damu na mwili,yeye naye vivyo hivyo alishiriki yayo hayo,ili kwanjia ya mauti amharibu yeye aliekuwa na nguvu za mauti,yaani,Ibilisi,awaache huru wale ambao kwamba maisha yao yote kwa hofu ya mauti walikuwa katika hali ya utumwa.)Ibilisi ameharibiwa hii sio kwamba hayupo.Hayupo lakini  amenyanganywa mamlaka yote na Yesu ndiye anayo sasa .Yeye alie ushindi wa kifo,neno lililotumika kuharibu kwakiyunani linaitwa  katargeo likiwa na maana ya kusababisha kutokuwa na uwezo,kutokuwa na umuhimu,kupoozesha.hivyo kwa kupitia kifo cha Yesu.

Sio kwamba amelipa adhabu ya dhambi tu bali alimfanya shetani  kutokuwa na uwezo,amemtiisha hadi kukosa nguvu amempoozesha kwahiyo ukimpokea Yesu huna haja ya kumuogopa ibilisi wala hukumu inayofuata baada ya kifo wala huogopi wachawi na kundi lake lote la giza. Ebrania9:27 anasema.Na kama  vile watu walivyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu. Ebr.10:27 bali kuna kuitazamia hukumu yenye kutisha,na ukali wa moto uliotayari kuwala wao wapingao Rumi8:1-2 Sasa basi hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu.Kwasababu sheria ya Roho wa uzima ule ulio katika Kristo Yesu imeniacha huru,mbali na sheria ya dhambi na mauti.Hapo ndipo  mauti ilipopoteza uchungu wake,usiogope matokeo ya kifo maana hakiwezi kuharibu nafsi na roho ya aliyeokoka  Kristo anamiliki.pamoja na hayo kama hukwenda sawa na elekezo la Neno la MUNGU ndio inakua mlango wa kuvuta laana ya BWANA.MITHALI 3:33 Laana ya Bwana I katika nyumba ya waovu bali huibariki maskani ya mwenye haki hebu uwe na ufahamu sahihi wenye haki ni ni wale walio amini kazi ya Mungu ya ukombozi kwa njia ya kifo cha Yesu. Gal 2;16 Hali tukijua ya kwamba mwanadamu hahesabiwi haki kwa matendo ya sheria,bali kwa imaniya Kristo Yesu;sisi tulimwamini Kristo Yesu ili tuhesabiwe haki kwa imani ya Kristo Yesu,wala si kwamatendo ya sheria;maana kwa matendo ya sheria hakuna mwenye mwili atakaye hesabiwa haki.ukifikia cheo hicho laana isiyo na sababu haikupiga. Maana yake ukiruhusu adui kupata sababu laana yaweza tenda kazi.mithali 26:2 kama shomoro katika kutangatanga kwake, na kama mbayumbayu katika kuruka kwake .kadhalika laana isiyo nasababu haimpigi mtu. Sasa fimbo ya enzi anayo Yesu iwapo tutatembea na kuitia Imani  {Rum 16:26
Laana aina ya tatu ni ya watumishi wa Mungu[Manabii] mfano Yoshua  6:26 “Naye Yoshua akawaapisha kiapo wakti ule,akasema,na laaniwe mbele BWANA mtu Yule atakayeinuka na kuujenga mji huu wa heriko;ataweka msingi wake kwa kufiliwa na mzaliwa wa kwanza wake,tena atasimamisha malango yake kwa kufiliwa na motto wake mwanamume aliye mdogo.” Joshua alipowaapisha kiapo wote waliyoenda kinyume na kiapo kile uharibifu uliwafika [2 samweli 1:21] Daudi alipokuwa analia aliongea maneno ambayo yanafanya kazi tangu alipoyanena hadi leo.Elewa Miaka elfu ya Daudi ndio Yesu akaja miaka Elfu mbili tangu Yesu aje hadi tulip oleo yale maneno bado yana nguvu,milima ya Gibea haina maongeo imedumu miaka elfu tatu
Inaendeleaaa……………………..